Search This Blog

Sunday, March 29, 2020

Fatma Karume amcharua Makonda kutangaza mtoto wa Mbowe ana Corona



Wakili wa kujitegemea, Fatma Karume amemcharua Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa kitendo cha kumtangaza mtoto wa Freeman Mbowe kuwa ni mgonjwa wa Corona.

“@makonda-paul huna mamlaka ya kumtaja mgonjwa kwa jina,” aliandika Fatma Karume katika ukurasa wake wa twitter.

Aliongezea kuwa “Ilikuwa upeleke Ambulance kwenda kumchukua awekwe Quarantine na si kumtaja hadharani,” aliandika.

Fatma aliandika ujumbe huo baada ya kuona Makonda anamjibu Waziri wa afya jamii na maendeleo, jinsia, wazee na watoto kwa kudai yupo sahihi kwa asilimia 100 kutangaza kwa kuwa ni mwenyekiti wa usalama mkoa wa Dar es salaam


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...