Search This Blog

Tuesday, March 17, 2020

China mbioni kuitambulisha chanjo ya virusi vya colona

Wizara ya Elimu nchini China imesema kuwa chanjo ya virusi vya Corona iliyogunduliwa na taasisi za elimu ya juu nchini humo, itafanyiwa majaribio ya kitabibu au kuanza kutumika haraka iwezekanavyo kuanzia mwishoni mwa mwezi Aprili.

Chanjo hiyo hivi sasa ipo katika majaribio kwa wanyama kwa ajili ya majaribio ya usahihi na ufanisi wake.

Kwa mujibu wa mmoja wa ofisa kutoka Wizara ya Elimu, Lei Chaozi, amesema itaanza kujaribiwa kwa waathirika au kutumika mwishoni mwa mwezi Aprili.

Wizara imevihimiza vyuo vikubwa nchini humo vikiwemo Peking University, Tsinghua University na Xiamen University pamoja na taasisi za utafiti wa kisayansi kuongeza kasi ya utafiti wa chanjo hiyo ili ianze kutumika kwa haraka.

Chanzo: Xinhua News.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...