Search This Blog

Thursday, March 26, 2020

Burundi Yakanusha Taarifa Inayosambaa Mitandaoni Kwamba Haina Vifaa Vya Kupima Corona

Burundi imedai watu wanaotumia mtandao wa internet kusema nchi hiyo haina vifaa vvya kugundua virusi vya corona kuwa ni waongo.

Kwenye taarifa iliyotolewa jana jioni, msemaji wa serikali ya Burundi Prosper Ntahorwamiye amesema nchi hiyo ina vifaa vya kutosha na vyenye ufanisi vya kugundua virusi vya corona. 

Ametolea mfano ushahidi kuwa mwalimu kutoka shule inayomilikiwa na Wafaransa aliyeshukiwa kuwa na virusi hivyo amepimwa, lakini matokeo yameonesha kuwa hana virusi.

Serikali ya Burundi imeonya dhidi ya vitendo vya kupotosha ukweli na kutafsiri vibaya maamuzi yaliyotolewa na serikali. 

Msemaji huyo amesema serikali ina madaraka ya kuchukua hatua mwafaka dhidi ya watu wanaotoa kauli zisizo za kweli.

Wakati huohuo, serikali ya Burundi imeshukuru China kwa kutoa vifaa vya kuisaidia kukabiliana na uwezekano wa mlipuko wa virusi vya Corona nchini humo.

Credit: CRI


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...