Search This Blog
Sunday, March 1, 2020
Afrika Kusini Yaona Isiwe TABU Kuwarejesha Raia Wake 151 Kutoka Wuhan China
Afrika Kusini inapanga kuwarejesha nyumbani raia wake 151 kutoka mji wa Wuhan nchini China, wakati virusi vya Corona vikizidi kusambaa duniani kote.
Raia hao watarejeshwa katika operesheni ya kijeshi na kisha kuwekwa katika karantini kwa siku 21 baada ya kuwasili nchini humo, amesema waziri wa afya Zweli Mkhize.
Raia wote watakaorejeshwa ni wazima wa afya na hawajaambukizwa virusi hivyo. Uamuzi wa kuwarejesha nyumbani unafuatia maombi ya familia za raia hao waliokwama Wuhan, mji unaotajwa kuwa chanzo cha mripuko.
HIZI HABARI KAMA HIZI ZINAPATIKANA KWENYE APP YA UDAKU SPECIAL DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG <DOWNLOAD HAPA>
Kwa mujibu wa waziri wa afya, Afrika Kusini imejiandaa kukabiliana na virusi hivyo na imetenga hospitali kadhaa za umma ili kushughulikia uwezekano wa maambukizi.
Taifa hilo halijathibitisha kisa chochote cha virusi vya Corona ndani ya mipaka yake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment