Search This Blog

Saturday, February 8, 2020

YANGA YAENDELEA KUMFUKUA 'MWIZI' KIMYA KIMYA.

Yanga Africa yaendelea kumfukuza mwizi kimya kimya maara baada ya leo kuendelea kugawa vipigo mfululizo dhidi ya wazee wa kupapasa Ruvu Shooting ya Mlandizi Mkoani Pwani.

Yanga ilitumia dakika 40 za mchezo katika kipindi cha kwanza kupata bao la kuongoza na la ushindi katika mtanange huo mkali mara baada Papaa Davido Molinga kumalizia kwa kichwa krosi iliyopigwa na Ditram Nchimbi na kumshinda mlinda mlango wa Ruvu Shooting Mohamed Makaka.

Yanga sasa wanajikusanyia alama 37 katika michezo 18 ya ligi kuu Tanzania bara huku ikishika nafasi ya tatu nyuma ya vinara wa ligi wekundu wa msimbazi we alama 50 katika michezo 20.
Kikosi cha Ruvu ShootingKikosi cha Yanga SC.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...