Search This Blog

Monday, February 10, 2020

Wanajeshi wa Marekani walioathirika ubongo kutokana na shambulio la Iran wafikia 109


Idadi ya wanajeshi wa Marekani wanaougua majeraha ya ubongo kufuatia shambulio la Iran dhidi ya wanajeshi wa Marekani katika kambi moja nchini Iraq mwezi Januari imefikia 109, kulingana na maafisa wa Marekani.

Idadi hiyo iliongezeka kutoka wanajeshi 64 walioripotiwa hapo awali na Pentagon. Rais Donald Trump awali alisema kwamba hakuna raia wa Marekani waliojeruhiwa wakati wa shambulio hilo.

Shambulio hilo la tarehe 8 mwezi Januari linajiri huku kukiwa na wasiwasi kuhusu mauaji ya jenerali mmoja wa Iran. karibia asilimia 70 ya wanajeshi waliojeruhiwa wamerudi kazini , pentagon iliongezea katika taarifa.

Ongezeko la visa vilivyoripotiwa linatokana na majeraha madogo ikimaanisha kwamba dalili huchukua muda kujitokeza , Pentagon ilisema katika mkutano na vyombo vya habari mwezi Januari.

Mbunge wa chama cha Republic nchini Marekani Joni Ernst alitoa wito wa kutolewa kwa majibu zaidi siku ya Jumatatu.

''Ni muhimu kuwa na mpango wa kuwatibu hawa waliojeruhiwa'' .

"Nimetoa wito kwa Pentagon kuhakikisha usalama na utunzaji wa vikosi vyetu vilivyopelekwa ambao wanaweza kuwa na majeraha ya mlipuko nchini Iraq," aliandika katika twitter.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...