Search This Blog

Monday, February 10, 2020

Rais Magufuli Kuzindua Rasmi Wilaya Ya Kigamboni Leo

Rais Magufuli leo February 11 kuanzia Saa Mbili Asubuhi anatarajiwa Kuzindua Rasmi Wilaya Mpya ya Kigamboni ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza kwa Wingi katika Uzinduzi huo wa Kihistoria.
 
RC Makonda amesema hafla ya Uzinduzi huo inatarajiwa kuanza Saa Moja Asubuhi kwenye Viwanja vya Mkuu wa Wilaya ambapo Rais Magufuli atazindua Jengo la Utawala la Mkuu wa Wilaya, Jengo la Halmashauri na Majengo ya Hospital ya Wilaya ya Kigamboni.
 
Uzinduzi huo unakuja wakati muafaka ambao Tayari Serikali imefanya juhudi kubwa za Maendeleo katika Wilaya hiyo kupitia Miradi mbalimbali ikiwemo Ujenzi wa Barabara za Lami, Ujenzi wa Hospital, Vituo vya Afya, Zahanati, Huduma za maji, Elimu pamoja na huduma zote muhimu.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...