Search This Blog

Sunday, February 23, 2020

Radi yaua mwingine Njombe akiwa ananyoa nywele saluni


Na Amiri kilagalila, Njombe

Martin Nyigu (35) mkazi wa kijiji cha Lusitu,kata ya Luponde,halmashauri ya mji wa Njombe,mkoani Njombe amefariki dunia kwa kupigwa na radi leo majira ya saa 9 alasiri akiwa ananyoa nywele saluni huku kinyozi na wateja waliokuwa wanasubiri huduma wakiwa salama.

Akizungumza na Muungwana blog diwani wa kata ya Luponde Ulrick Msemwa amethibitisha ukweli wa taarifa hizo kwa mujibu wa taarifa za awali alizopokea kutoka kwa mtendaji wa kata ya Luponde Patrick Mtundu.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...