Search This Blog
Sunday, February 9, 2020
Nzige waripotiwa kuingia Tanzania
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro nchini Tanzania Anna Mgwira amethibitisha kuonekanwa kwa kundi la nzige katika baadhi ya vijiji vya Moshi.Wadudu hao wanaaminika kutokea upande wa nchi ya Kenya ambayo inapakana na Tanzania. Awali kulikuwa na taarifa zilizoenea katika mitandao ya kijamii na kusema kundi la nzige limeonekana umbali wa kilomita 50 kutokea mpaka wa Tanzania na Kenya.
Anna Mghwira anasema walipopata taarifa hizo asubuhi, waliangalia zaidi upande wa maeneo ya Taveta, lakini baadae taarifa zikaonyesha wameonekana katika baadhi ya vijiji vya Moshi."Sisi tulipopata hizo habari asubuhi, tukawa tunaangalia maeneo ya jirani yetu na Taveta, na ikaonekana upande ule hakuna, lakini jioni hii kumetokea taarifa zinazoonyesha kuwa maeneo ya Moshi hao nzige wameonekana kabisa sio kwamba wako km 50.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment