Search This Blog
Saturday, February 15, 2020
JE, Wajua Asili ya NENO Msela na Baharia Kutumika Mtaani?
Inadaiwa Msela ilitokana na neno, ‘Sailor’ mfanyakazi wa meli ambaye sio ofisa au baharia wa kawaida. Huyu ni mtu ambaye alikuwa anasafiri sana na meli kipindi hicho. Waliokuwa wanasafiri wakaita m-sailor, neno hilo likaja kuwa Msela
Miaka ya nyuma watu walikuwa wakijiita ‘masela’ kutokana na kuwaiga watu waliokuwa wamepanda meli na kwenda Ulaya
Walikuwa wakirudi Tanzania wanakuja na vitu vya thamani. Pia walipenda kuninginiza cheni na miondoko yao ilikuwa ni kudunda kutokana na kuishi kwenye meli ambapo muda mwingi walikuwa wakivaa viatu vikubwa na ile hali ya chombo kuyumba kutokana na wimbi
Kipindi cha sasa vijana wengi wanajiita "Baharia" hii ni kutokana na mabaharia kuwa watu wa kusafiri kila eneo, kusaidiana, kuweka kambi popote na kuwa na mahusiano ya kimapenzi kila sehemu atayofika, walikuwa wakitumia msemo wa "New Port, New Wife"
Hii imepelekea sasa vijana wengi mtaani na kwenye kada mbalimbali kutumia neno la baharia au kujiita baharia
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment