Search This Blog

Sunday, February 9, 2020

Inter yaimiminia mvua ya mabao AC Milan

Rome, Italia. Antonio Conte amepania kutwaa ubingwa wa Italia msimu huu baada ya kuendeleza rekodi ya kushinda katika mechi zake.

Ushindi wa jana wa mabao 4-2 dhidi ya watani wao wa jadi AC Milan umeifanya timu hiyo kucheza mechi 16 bila kupoteza.

Inter Milan imekwea hadi nafasi ya kwanza na kuiporomosha  Juventus ambayo imekuwa kileleni muda mrefu.

Kocha huyo alisema anataka kutimiza ndoto ya kuipa ubingwa Inter Milan licha ya kukabiliana na upinzani mkali dhidi ya Juventus na Lazio.

“Tuna ndoto. Tumekuwa tukiimarika kutoka mchezo mmoja hadi mwingine. Hawa vijana wamekuwa wakifanya kazi nzuri,” alisema Conte.

Inter Milan Jumatano keshokutwa itakuwa nyumbani Napoli kabla ya kupepetana na wapinzani wao wanaowania ubingwa huo Lazio.

Advertisement

Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Romelu Likuku ameendelea kung’ara baada ya kufunga bao. Inter Milan na Juventus zina pointi 54 zikifuatiwa na Lazio (53) na Atalanta (43).

Let's block ads! (Why?)

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...