Search This Blog

Tuesday, February 18, 2020

Hakuna viza kwa afanyakazi wasiokuwa na ujuzi Uingereza

Wafanyakazi wasiokuwa na ujuzi hawatapata viza chini ya mpango mpya wa uhamiaji wa serikali baada ya Uingereza kujiondoa katika Muungano wa Ulaya.

Serikali inahamasiha waajiri kuacha kutegemea wafanyakazi wa kulipwa mshahara wa chini kutoka Ulaya na kuwekeza zaidi katika kudumisha wafanyakazi na kuendelezea teknolojia.

Wizara ya mambo ya ndani imesema Ulaya na raia wa nchi ambazo sio wanachama wa Muungano huo watakuwa wanachukuliwa walio katika daraja moja baada ya usafiri huru kati ya Uingereza na Muungano wa Ulaya kufikia ukomo wake Desemba 31.

Makampuni yanasema sheria kali kama hizo zitafanya iwe vigumu kuvutia wafanyakazi.

Lakini waziri wa mambo ya ndani Priti Patel amesema utekelezaji wa mfumo mpya kutamaanisha watu wenye weledi tu ndio watakaoingia Uingereza.
 


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...