Search This Blog

Saturday, February 8, 2020

Guterres asema uvamizi wa nzige unahusiana na mabadiliko ya hali ya hewa

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema upo uhusiano kati ya mabadiliko ya hali ya hewa na nzige waliovamia nchini Ethiopia na katika eneo la Afrika Mashariki.

Guterres ameyasema hayo mjini Addis Ababa kabla ya mkutano wa kilele wa nchi za Umoja wa Afrika unaoanza hii leo.

Mada kuu ya mkutano huo wa 33 ni usalama. Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema uvamizi wa wadudu hao ni mbaya zaidi kuwahi kutokea Afrika Mashariki mnamo kipindi cha miaka 25.

 Ameelezea wasiwasi wake kwamba uvamizi huo unaweza kusababisha baa la njaa katika nchi ambazo tayari zinapambana na ukosefu wa chakula.

Nchi zilizoathirika kutokana na uvamizi wa nzige ni Ethiopia, Somalia, Kenya, Eritrea na Sudan huku kukiwa na kitisho cha wadudu hao kuenea hadi Uganda na Sudan Kusini.

Kuhusu mkutano, Guterres amesema anaamini kwamba ukosefu wa utulivu katika eneo la Sahel na nchini Libya utapatiwa ufumbuzi na kwamba Umoja wa Mataifa unaziunga mkono juhudi za nchi za Afrika.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...