Mtoto mwenye umri wa miaka 13 ambaye alikuwa akisoma katika Shule ya Msingi Msakila Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi, amekatishwa masomo yake akiwa darasa la 3 kwa kupewa ujauzito ambao sasa una miezi saba na mtu aliyefahamika kwa jina la Salum Mayunga dereva bodaboda.
Akizungumza kwa masikitiko makubwa mtoto huyo amesema kuwa, wazazi wake wote wawili walifariki na kuchukuliwa na ndugu ambao walimwambia aende akaishi na kijana huyo, bila kujali ni mwanafunzi na pia umri wake ni mdogo.
Consolata Mlaponi ni mmoja kati ya watu waliojitolea kumsaidia mtoto huyo ambapo amesema kuwa kwa sasa mtoto huyo anakabiliwa na hali ngumu ya kimaisha, ikilinganishwa na umri wake ambao ni mdogo na hawezi kujitafutia.
Huku Jeshi la Polisi mkoani humo likianzisha oparesheni kabambe yenye lengo la kuwabaini na kuwakamata wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment