Search This Blog

Tuesday, February 11, 2020

Beckham amaliza mchezo, Neymar kutua Inter Miami

DAVID Beckham amekamilisha bonge la dili katika klabu yake ya Inter Miami baada ya kufanikiwa kunasa saini ya straika wa Paris Saint Germain, Neymar, ambaye amekubali kutua kwenye klabu hiyo ya Ligi Kuu Marekani miaka 10 ijayo.

Wakati Barcelona na Real Madrid zikipambana kuisaka saini yake, Mbrazil huyo amefanya makubaliano na Beckham ambaye ni mmiliki wa Inter Miami kuwa atajiunga na timu hiyo kabla ya kustaafu.

Dili lenyewe lilikuwa hiv, wawili hao walikuwa wamekaa wakipiga stori huku tukio hilo likirushwa moja kwa moja na Cheneli ya YouTube, OTRO, ndipo Beckham alipompa Neymar karatasi isiyo na kitu na kumtaka asaini iwe kama makubaliano kutua Inter miaka 10 ijayo.

Licha ya Beckham kumwambia Neymar timu yake hailipi pesa ndefu, lakini alikubali.

Let's block ads! (Why?)

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...