Search This Blog
Sunday, January 5, 2020
Wanafunzi wauawa kwa bomu wakiwa ndani ya basi
Watu 14 wamepoteza maisha na wengine wanne wamejeruhiwa baada ya basi walilokuwa wanasafiria kulipuliwa kwa bomu, Kusini-Magharibi mwa Burkina Faso.
Basi hilo lilikuwa limebeba wanafunzi waliokuwa wanarejea mashuleni baada ya kumaliza mapumziko ya sikukuu za kuukaribisha mwaka mpya 2020.
Taarifa zilizotolewa na vyombo vya usalama nchini humo zimeeleza kuwa basi hilo lilikanyaga bomu katika eneo la Toeni.
Ingawa bado watuhumiwa wa tukio hilo hawajafahamika, nchini humo kumekuwa na ongezeko la tishio la makundi ya kigaidi.
Katika siku ya Christmas, raia 35 waliuawa katika matukio ambayo yalidaiwa kutekelezwa na makundi ya kigaidi dhidi ya kambi za jeshi.
Nchi za Afrika Magharibi zimeendelea kupambana na vitisho vya kigaidi lakini mauaji na vitendo vya kigaidi vinaendelea.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment