MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa tahadhari ya kuwapo kwa siku mbili za mvua kubwa kwenye mikoa saba kuanzia jana.
Mikoa itakayopata mvua hiyo kwa mujibu wa TMA ni Singida, Rukwa, Mbeya, Iringa, Njombe, Songwe na Dodoma.
Meneja wa Utabiri kutoka Kituo Kikuu cha Utabiri TMA, Samuel Mbuya, aliwataka wakazi wa mikoa hiyo kuchukua tahadhari.
"Ni vyema watu wakachukua tahadhari ikiwamo kuzibua mifereji ili kuruhusu maji yasituame sehemu moja, maana hiyo ndiyo chanzo cha mafuriko, lakini pia kuhakikisha wanawahi kwenda kwenye maeneo yao ya kazi na kuondoa msongamano barabarani," alishauri.
Kwa mujibu wa meneja huyo, mamlaka itaendelea kutoa tahadhari, angalizo na taarifa mbalimbali za hali ya hewa kwa wananchi, ili kuwakinga na majanga yanayoweza kutokea kwenye jamii.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment