Search This Blog

Sunday, January 12, 2020

Salamba: Ushirikiano ninaopewa na wachezaji wenzangu ni mkubwa

ADAM Salamba, mtanzania anayekipiga kwa sasa ndani ya timu ya Al-Jahra SC, iliyopo Uarabuni amesema kuwa ushirikiano anaopewa na wachezaji wenzake ni mkubwa.

Akizungumza na Saleh Jembe, Salamba amesema kuwa amekuwa akifurahia maisha ya huko kutokana na ushirikiano anaopewa na wachezaji wenzake.

"Huku ninaishi vizuri na wenzangu, tunashirkiana vema na kila mchezaji jambo ambalo linanifanya niwe na furaha.

"Nafanya yote kutokana na kupenda kazi yangu, nipo huku ila napeperusha vema bendera ya Tanzania kwani wengi wanapenda kutambua habari za nyumbani," amesema Salamba.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...