Search This Blog

Saturday, January 11, 2020

Rais Magufuli kuunga mkono jitihada za wawekezaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli  amesema Serikali zote mbili ya Mapinduzi ya Zanzibar na ya  Muungano itashirikiana kwa pamoja kuwaunga mkono wawekezaji ili nchi ipate maendeleo.

Hayo  ameyasema huko  katika Hoteli ya Verde Mtoni wakati wa ufunguzi wa Hotel hiyo  ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za kuadhimisha miaka 56 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar  ambayo yamemkomboa Mzanzibar.

Alisema wawekezaji wanaowekeza katika visiwa hivi kwa sababu ya amani na utulivu ulikuwepo jambo ambalo linawapa imani ya kuekeza na  kujipatia Maendeleo nchini .

Pia alisema Mapinduzi ya 1964 ilikuwa na lengo la kuuondowa utawala  dhalimu wa Kisultani kwa kujipatia uhuru wa nchi na kuweza kujiongoza  wenyewe kwa kujipatia maendeleo mbali mbali kupitia miradi ya ikujenga ustawi wa nchi .

 Aidha alimpongeza mmiliki wa hoteli hiyo kwa kuwekeza kwani kufanya hivyo kutaweza kupatikana fursa za kufikia  watalii wengi na kuzidisha pato kwa Serikali  pamoja na vijana kujipatia ajira .

 Hata Hivyo alisema fursa ziko nyingi Zanzibar na amewataka wawekezaji waendelee kuwekeza mbali ya kukuza utalii , zipo fursa nyengine kama kilimo na uvuvi na mambo mengine ya maendeleo.

Vile vile alisema wawekezaji ambao wanaoekeza ni vyema kutoka ndani ya nchi yao sio kutoka nje ya nchi na serikali inaahidi kutoa mashirikiano, ijapokuwa wanaviazio vidogo vya mtaji wao .

“wawekezaji sio watoke nchi za nje bali wajitokeze wa ndani ya nchi na Serikali itawapa mashirikiano,  wala wasikate tamaa, kwani hata Mwekezaji  huyu alianzia chini hadi sasa yuko juu”,alisema Magufuli.

Nae Waziri wa Fedha na Mipango Mohamed Ramia Abdilwawa amesema hoteli hiyo imejengwa kwa uzalendo na inaonyesha njia ya kujipatia maendeleo katika Nyanja mbali mbali za kuingiza pato kwa Serikali.

Pia amempongeza muwekezaji huyo kwa kulipa kodi kwa wakati na kuwaomba wawekezaji wengine wawe na tabia kama hiyo kwani kulipa kodi kwa wakati kunaengeza pato la Serikali .

Amesema wawekezaji wazalendo wanapata fursa ya kuwekeza na kuzidisha uchumi wa Nchi, hayo ndio malengo ya Mapinduzi Matukufu katika kuimarisha maendeleo.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bakhressa Group of Companies Salim Azizi Salim akitoa maelezo mafupi ya hoteli kutoka kwa mmiliki wa mradi amesema hotel hiyo imejengwa ya  kisasa na ina kila aina ya kuvutia kwa watalii ikiwemo sehemu za kuogelea na ina vyumba 106.

Pia alisema fursa nyingi zimetoka za ajira ambapo zaidi ya nafasi 250 zimetolewa kwa wananchi  na wameweka sehemu nyingi za vivutio kiwemo sehemu za watoto za kusherehekea sikukuu.

Mmiliki huyo alimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dkt Ali Mohamed Shein kwa  uongozi wake wa busara katika nchi na kuendeleza yale mazuri yote ya Mapinduzi yaliyoanzishwa tokea  mwaka 1964.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...