Search This Blog

Tuesday, January 14, 2020

Manara: Yaliyotokea ni historia isiofaa kurejewa sasa tuelekeze akili zetu Mwanza

Ofisa habari wa timu ya wekundu msimbazi Simba bwana Haji Manara ametoa hisia zake za maaumivu juu ya kufungwa na amewaomba radhi wanasimba na kusema kuwa hilo kwao ni funzo.

Kupitia instagramu yake ameandika hivi;

Wanasimba wenzangu!!
Najua maumivu mliyopitia jana na nnafahamu karaha mnazopata toka kwa watani zetu, lakini niwaambie kitu kimoja, hili kwetu ni funzo, ni funzo kwa kila mmoja klabuni.

Viongozi,Benchi la ufundi na hata wachezaji wetu.

Wanasimba wa leo hawapo tayari kufungwa na hasa kama unafungwa kirahisihisi.

Kocha wetu atakuwa kaelewa nn mnataka wenye timu na wachezaji bila shaka watapambana ili kuwapa Wanasimba mnachostahili
Mm imani yangu ni kubwa sana kwao, hakuna shaka yaliyotokea jana ni historia isiyofaa kurejewa.

Sote tunaumia lakini hii ndio Raha na karaha za football, mtu wa mpira lazma upitie tamu na chungu za kushabikia soka.

Now akili yetu tuelekeze Mwanza ktk mechi mbili ngumu zijazo.

Tushirikiane kupata points sita za CCM kirumba
Insha'Allah tutafanikiwa

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...