Search This Blog
Tuesday, January 21, 2020
Kauli ya Lipumba baada ya Madiwani CUF kuhamia CCM
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Prof. Ibrahim Lipumba, amesema anashangazwa na kitendo cha Madiwani 8 wa Halmashauri ya jiji la Tanga waliojiengua chama hicho na kusema viongozi hao wamekwenda kuunga hali ngumu ya maisha.
Profesa Lipumba ameyasema hayo katika kikao cha ndani cha wanachama kilichofanyika jijini Tanga.
Lipumba amesema kuwa "kila mmoja analalamika kwamba vyuma vimekaza wao wanakwenda kuunga mkono vyuma vimekaza, hii ni ajabu sana"
Mwenyekiti huyo aliwapongeza Madiwani waliokataa kuyumbishwa na kusisitiza kwamba msimamo huo ndiyo utakaowasababisha wananchi kuwachagua tena katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2020.
Hivi karibuni akiwa mkoani Tanga Katibu Mkuu wa CCM, Bashiru Ally aliwapokea Madiwani 8 akiwemo Naibu Meya wa jiji la Tanga.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment