Search This Blog
Friday, January 24, 2020
Hukumu yatolewa kwa watanzania waliozamia Afrika kusini
Watanzania 16 wamehukumiwa kifungo cha Miezi Sita (6) jela au faini ya Tsh. 300,000 kila mmoja baada ya kukiri kuzamia Nchini Afrika Kusini kinyume na taratibu zilizowekwa na Idara ya Uhamiaji.
Wengine 14 wamehukumiwa kifungo cha miezi 18 au faini ya Sh 50,000 kila mmoja, baada ya kukiri kosa hilo.
Watuhumiwa hao walirudishwa nchini na kufikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ambapo walikiri mashtaka yaliyokuwa yanawakabili. Hakimu Agustina Mbando alitoa hukumu hiyo kutokana na makosa hayo kujirudia.
Awali, Wakili wa Serikali, Godfrey Ngwijo, aliomba Mahakama kutoa adhabu kali na kusema utaratibu wa kutoka nje ya Nchi unafahamika.
Kwa mujibu wa Wakili huyo, washtakiwa waliondoka nchini Kinyume cha Kanuni za Uhamiaji namba 20 (3) (a) G.N namba 657 ya mwaka 1997 inayosomwa pamoja na kifungu namba 48 (2) ya Sheria ya Uhamiaji namba 54 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment