Search This Blog

Monday, January 6, 2020

Chalamila apiga marufuku matangazo ya waganga wa jadi atoa maagiza polisi

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, amewaagiza Polisi Mkoani humo kuyaondoa mabango yote ya waganga wa jadi yaliyobandikwa Mitaani yakiwemo yanayoeleza kuhusu kuongeza nguvu za kiume kwa madai kuwa yanawaingiza Wananchi kwenye majaribu ya kishirikina.

Chalamila amesema baada ya kuyaondoa mabango hayo, uanze mchakato wa kuwakamata waganga wa jadi wote wanaokiuka taratibu za Nchi na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola.

"Vijana wetu wameingia kwenye mitego ya ajabu, wanafikiri nguvu za kiume zinapatikana kwa Waganga mwisho wa siku wanaharibu miili yao na wanaingia kwenye ushirikina ambao hauna maana" - RC Chalamila

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...