Search This Blog

Monday, January 6, 2020

Aunt Ezekieli afunguka kuhusu kupungua kwa Wema

Muigizaji wa filamu nchini Aunty Ezekiel, amefunguka kuwa anapenda muonekano alionao rafiki yake Wema Sepetu, ila kwa upande wake amesema hana mpango wa kupungua kwa sababu ameridhika na jinsi alivyo.

"Muonekano wake nauona upo poa, hata mimi naona nakaa kwa shida kwa sababu ya ubonge  kwa yeye alivyopungua nimependa, ila mimi sina mpango huo kwa kweli nipo poa kwa hivi nilivyo, kama kupungua labda iwe kidogo tu lakini kupungua zaidi sijawahi kuwaza" amesema Aunty Ezekiel.

Aidha Aunty Ezekiel akizungumzia hofu yake ya kupungua amesema,
"Sihofii chochote ila naamini mimi kama tayari ni mama wa mtoto, kwahiyo waswahili wanasema ukiingia leba kuna viungo lazima vibadilike, haviwezi kubaki vile vile na vitu vingine ukivilazimisha inakuwa shida, kwahiyo naukubali huu mwili ukizingatia bado nahitaji kuwa mama zaidi" ameongeza.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...