Search This Blog

Thursday, December 26, 2019

Wasudan Washerehekea Krismasi Baada ya Miaka 70



Kwa mara ya kwanza Serikali ya Sudan imeruhusu sikukuu ya Krismasi kuadhimishwa nchini humo baada ya miaka sabini.

Siku hiyo imesherehekewa na asilimia tatu ya watu ambao ni wakristo nchini humo huku asilimia 97 ya waliobaki ni waislamu.

Kuruhusu mapumziko ya siku ya Krismasi ni miongoni mwa mabadiliko makubwa ambayo yameanza kuonekana baada ya kuingia madarakani kwa kiongozi mpya, kufuatia kuondolewa kwa Rais wa zamani Omar al-Bashir mwezi Aprili.

Waziri anayeshunghulikia masuala ya dini Nasrudin Mufreh, amesema hatua hiyo imekuja baada ya katiba mpya kuruhusu Uhuru wa kuabudu.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...