Search This Blog
Monday, December 30, 2019
Wapiganaji Wanne wa Kundi Al Shabaab Wauawa Somalia
Wapiganaji wanne wa kundi la kigaidi la Al-Shabaab nchini Somalia wameuawa kwenye mashambulizi ya anga yaliyofanywa na majeshi ya Marekani katika maeneo mawili kwenye miji ya Qunyo na Caliyoow.
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi la Marekani mashambulizi hayo yalifanyika siku moja baada ya takriban watu 90 kuuawa katika shambulizi la bomu lililotegwa ndani ya lori kwenye kituo cha ukaguzi chenye pilika pilika nyingi katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
Marekani hufanya mashambulizi ya anga mara kwa mara nchini Somalia katika juhudi za kuisaidia serikali dhaifu, inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa iliyo katika mji mkuu wa Mogadishu na ambayo imekuwa ikipigana na kundi la Al-Shabaab kwa miaka kadhaa sasa.
Kamandi ya jeshi la Marekani barani Afrika, AFRICOM imesema serikali za Marekani na Somalia zitaendeleza mapambano dhidi ya makundi ya kigaidi kwa lengo la kuyadhoofisha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment