Search This Blog
Sunday, December 29, 2019
Viongozi wa Somalia na UN walaani vikali shambulizi la kigaidi Mogadishu
Viongozi wa serikali ya Somalia na Umoja wa Mataifa (UN) wamelaani vikali shambulizi la kigaidi lililotokea Mogadishu, Somalia na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 80 na wengine 149 kujeruhiwa hadi sasa.
Msemaji wa serikali ya Somalia Ismael Mukhtar Omar amethibitisha idadi ya vifo hivyo vilivyotokana na lori lililotegwa bomu kulipuka katika kituo cha ukaguzi wa usalama katika barabara ya Afgoye iliyopo viunga vya Mogadishu.
Kwa mujibu wa Bw. Omar, miongoni mwa watu waliokufa wamo wanafunzi takriban 15 wa chuo kikuu cha Banadir.
Afisa wa polisi aliyepo kwenye eneo la tukio amesema mlipuko huo uliolenga ofisi ya kodi ya mapato ulitokea ghafla wakati polisi wanakagua gari zinazopita barabarani na kusababisha vifo na uharibifu mkubwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment