Search This Blog
Monday, December 9, 2019
Nchi ya Saudi Arabia yaruhusu migahawa kuwa na mlango mmoja kwa ajili ya jinsi zote
Hatimae Serikali nchini Saudi Arabia, imeruhusu migahawa kuwa na mlango mmoja wa kuhudumia wateja bila kuzingatia jinsia ama familia, ambapo hapo awali ilikuwa lazima kuwa na mlango mmoja kwa ajili ya familia wa wanawake na mwingine wa wanaume.
Sharti hilo kwa sasa limeondolewa, huku migahawa mingi pamoja na maeneo mengine ya kufanyia mikutano ikifuata mkondo huo.
Mapema mwaka huu, agizo kutoka kwa Mfalme lilihitaji wanawake wa Saudia, kuruhusiwa kusafiri hadi Mataifa ya nje bila ya kupata ruhusa ya msimamizi wa kiume, pamoja na kuondoa marufuku ya wanawake kujiendesha wenyewe ambayo ilifikia ukomo wake mwaka 2018, iliyokuwa imedumu kwa miongo kadhaa.
Hata hivyo wanaharakati wanalalamika kwamba, sheria nyingi zinazobagua wanawake bado zinaendelezwa na watu wengi mashuhuri wanaotetea haki za wanawake, wamekamatwa hata wakati ambapo Serikali inafanya mabadiliko haya.
Tangu Mohammed bin Salman alipotawazwa na kuwa Mfalme mwaka 2017, amefanya mabadiliko katika jamii ambayo imekuwa ikikumbatia tamaduni zake za jadi.
Mabadiliko yake yameungwa mkono na jamii ya kimataifa lakini yamekuwa yakikandamizwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment