Search This Blog
Sunday, December 8, 2019
Mwafrika Atwaa Taji La Miss Universe 2019, Mtanzania Chali
Usiku wa kumkia leo Tarehe 9, Desemba 2019 Mrembo Zozibini Tunzi kutoka Afrika ya kusini amefanikiwa kunyakuwa taji la Miss Universe mwaka 2019
Shindano hili kilofanyika Nchini Ufilipino katika jiji La Madila likishirikisha jumla ya warembo 90 kutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni
Zozibini alifanikiwa kuingia tatu bora na kuwashinda wenzake wawili kutoka Puerto Rico Madison Anderson (Amekuwa mshindi wa pili) na Sofía Aragón kutoka Mexico ambaye amekuwa mshindi wa tatu
Zozibini amechukua mikoba ya taji hilo kutoka kwa raia wa Ufilipino, Catriona Gray ambaye alilitwaa mwaka 2018.
Zozibini anakuwa raia wa tatu wa Afrika Kusini kutwaa taji hilo baada ya Margaret Gardiner mwaka 1978, and Demi-Leigh Nel-Peters mwaka 2017.
Tanzania iliwakirishwa na mrembo Shubila Stanton ambaye hakufanikiwa kufika kwenye kumi bora ya mashindano hayo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment