Search This Blog
Monday, December 9, 2019
Madalali watakiwa kujitokeza katika uongozi wa chama cha TACA kujisajili
Madalali nchini wametakiwa kujitokeza katika Chama Cha Madalali TACA kwaajili ya kusajiliwa ili waweze kutambuliwa rasmi na kuondokana na utapeli unaoendelea kwa baadhi ya watu wanaojiita madalali.
Ameyasema hayo leo Mwenyekiti wa Chama Cha Madalali Tanzania TACA, Bw.Phidel Katundu katika kikao na Wanahabari katika ofisi ya Chama hicho Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika mkutano huo Bw.Katundu amesema kuwa wanampango wa kuwasajili madalali kwenye chama chao na mwisho watawakagua kila mwaka kwasababu kuna leseni zingine zinakuwa zimefika mwisho.
“Tunampango kila ifikapo mwezi Januari tunamkagua kila mwanachama kuna anavibali vyote ikiwemo kulipa kodi Serikalini ama leseni zinazomruhusu kuwa dalali na tukishajilizisha tunatoa cheti kwenye chama kwa mtu yeyote amtambue na kumpatia ushirikiano”. Amesema Bw.Katundu.
Aidha Bw.Katundu amesema kuwa changamoto kubwa ambayo inawakabili ni kuingiliwa na madalali ambao si rasmi yaani ambao wamekuwa matapeli na kuweza kuchafua sifa ya mwanachama wa TACA.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment