Search This Blog

Saturday, December 21, 2019

FIFA Yashusha Neema Tanzania


Shirikisho la soka nchini TFF limesema katika kukuza maendeleo ya soka la Tanzania, FIFA wapo kwenye mpango wa kujenga vituo vya michezo hapa nchini.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia ameyasema hayo leo kwenye mkutano mkuu wa TFF unaofanyika jijini Dar es salaam, ambao umehudhuriwa na wadau mbalimbali wa mpira.

Rais huyo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) amesema kuwa FIFA wameahidi kujenga uwanja mmoja hapa nchini.

England kujipima kwa Italia kabla ya Euro 2020
“FIFA wameahidi kujenga uwanja mmoja hapa nchini na tumekubaliana kujenga vituo viwili vya Soka (Technical Centres) kwa maeneo ya Tanga na Kigamboni-Dar es Salaam, ujenzi ambao mchakato wake umeshaanza na mapema mwakani ujenzi utaanza,” amesema Karia.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...