Search This Blog
Wednesday, December 18, 2019
BREAKING: Mbowe ashinda uchaguzi CHADEMA, Lissu apita Makamu Mwenyekiti
Freema Mbowe amefanikiwa kutetea nafasi ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) Taifa kwa kupata ushindi wa asilimia 93.5.
Mbowe aliyepata kura 886 amemshinda Cecil Mwambe aliyepata kura 59 pekee sawa na asilimia 6.2 huku kura 3 zikitajwa kuharibika.
Tundu Lissu ameshinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti Taifa (Bara) baada ya kupata kura 930 sawa na 98.8% akimshinda Sophia Mwakagenda (aliyetangaza kujitoa akiwa ukumbini) aliyepata kura 11 sawa na 1.2%.
Said Issa Mohamedi ameshinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa (Zanzibar) nafasi ambayo ilikuwa na mgombea mmoja.
Matokeo yote ya uchaguzi CHADEMA ni kama yanavyoonyesha chini.
MWENYEKITI WA TAIFA
1.Freeman Mbowe-886-93.5✔
2.Cecil David Mwambe- 59
3.HARIBIKA -3
MAKAMU MWENYEKITI BARA
1.Tundu Antipas Lissu-930-98.8%✔
2.Sophia H.Mwakagenda-11- 1..2%
HARIBIKA 9
MAKAMU MWENYEKITI ZANZIBARI
SAID ISSA MOHAMED
NDIYO 859-88.7%✔
HAPANA 95
HARIBIKA 1
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment