Search This Blog
Sunday, November 3, 2019
Siogopi kuongeza idadi ya wanaonichukia - RC Makonda
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa Mamlaka zinakula rushwa, haiwezekani mtu analalamikiwa lakini bado anapewa kazi.
RC Makonda kutokana na hilo amesema kuwa haogopi kuongeza idadi ya watu wanaomchukia.
Makonda alisema hayo katika ziara yake alipoingia kwenye mzozo na mkandarasi huyo ambaye alisema anafanya kazi kwa mujibu wa programu kama walivyokubaliana kitu ambacho kilionekana kumkera Makonda.
"Tanroads (viongozi wa Wakala wa Barabara) huyu Nyanza Road Works aliharibu mradi wa ujenzi barabara Temeke lakini mmempa tena kufanya mradi huu, kuna nini kinachoendelea?amehoji Makonda na kuongeza;
"Nasema mradi huu ndio wa mwisho. Sasa mumpe tena mradi mwingine mtanijua kama mimi ndio mkuu wa mkoa au nyie,"alisema na kumgeukia Ofisa Tawala wa Ilala, Jabiri Makame akimfokea.
Makonda alisema mkandarasi Nyanza Road Works ameharibu miradi mingi ikiwemo wa Nyakanazi kwenda Kakonko, Musoma na Temeke huku akishangaa kwa nini anaendelea kupewa miradi licha ya kuvurunda.
"Mamlaka zinakula rushwa, haiwezekani mtu analalamikiwa lakini bado anapewa kazi. Siogopi kuongeza idadi ya wanaonichukia, Nyanza Road Works tumempa zaidi ya sh milioni 800 lakini mpaka sasa anasuasua, vifaa hana ujanja ujanja tu,"amesema Makonda.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment