Search This Blog
Wednesday, November 6, 2019
Prof. Lipumba atuma ombi kwa Rais Magufuli
Profesa Ibrahim Lipumba ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) amemuomba Rais John Magufuli kuingilia kati suala la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kile alichokidai ni kuepusha vurugu na matatizo kwenye uchaguzi huo.
Ametoa kauli hiyo Dar es Salaam akizungumza na waandishi wa habari juu ya mwenendo wa shughuli za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, unaotarajia kufanyika Novemba 24, 2019.
"Kuepusha suala la vurugu kwenye Uchaguzi huu, naomba Rais Magufuli aingilie kati suala hili na wagombea walioenguliwa wapewe nafasi ya kuteuliwa kugombea".
Profesa Lipumba ameendelea kwa kusema,"Kitendo cha kuwanyima fomu wagombea wa upinzani sio tu halina tija kwenye ukuaji wa Demokrasia, pia ni matumizi mabaya na hela za umma, huwezi ukafanya semina, kuchapisha nyaraka mbalimbali huku ukijua hakuna uchaguzi bali wagombea wanapita bila kupingwa".
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment