Search This Blog

Sunday, November 24, 2019

NMB YAANDAA KONGAMANO LA SOKO LA HISA NA DHAMANA ZA SERIKALI KWA WEWEKEZAJI

 Meneja wa Masoko ya Fedha kutoka Benki Kuu (BoT), Bw. Lameck Kakulu (wa kwanza kulia) akielezea kuhusu soko la hisa Tanzania kwa wawekezaji mbalimbali wakati wa kongamano lililoratibiwa na Benki ya NMB jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Mkurugenzi wa utafiti, Sera na Mipango wa Mamlaka ya Masoko na Mitaji (CMSA), Alfred Mkombo, Meneja Mwandamizi wa huduma za Dhamana kutoka NMB, Bw. Avith Massawe na Mkurugenzi Mtendaji wa FIMCO Bw Ivan Tarimo.  
 Mweka Hazina wa Benki ya NMB, Aziz Chacha akiongea na wawekezaji wa Soko la Hisa na Dhamana za Serikali kuhusu huduma mpya ya uhifadhi wa dhamana na usimamizi wa uwekezaji katika masoko ya mitaji wakati wa kongamano lililoratibiwa na Benki ya NMB jijini Dar es Salaam.
Meneja Mwandamizi wa Huduma za Dhamana kutoka NMB, Bw. Avith Massawe akiwafunda wawekezaji wa soko la hisa na dhamana za serikali wakati wa kongamano hilo.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...