Search This Blog
Wednesday, November 13, 2019
Moto Ulioanzia Chumba cha Watoto Wateketeza Hospitali ya Mombasa
Hospitali ya Mombasa nchini Kenya imeteketea kwa moto, huku wagonjwa wakiokolewa na hakuna wagonjwa waliojeruhiwa na moto huo.
Imeelezwa kwamba moto ulizuka katika Hospitali hiyo yenye uwezo wa kulaza wagonjwa 125 majira ya saa 2:30 usiku wa kuamkia leo ambapo wauguzi 117 walikuwa hospitalini hapo wakiendelea na majukumu yao.
Kwa mujibu wa Kikosi cha Zimamoto, chanzo cha moto huo ulioanzia katika chumba cha watoto bado hakijafahamika.
Baada ya wagonjwa kuokolewa walikimbizwa katika hospitali jirani za Pandya, Aga Khan na Hospitali ya Coast General.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment