Aliyewahi kuwa Mrimbwende wa Taifa la Gambia mwaka 2014, Fatou Jallow amemtuhumu aliyekuwa Rais wa nchi hiyo, Yahya Jammeh kwa kumbaka na kumdharirisha.
Jallow ametoa tuhuma hizo mbele ya Tume ya Ukweli na Maridhiao na kusema kuwa Jammeh ambaye mwanzo alijifanya kama mzazi, akimpa zawadi na ushauri, alimlazimisha amkatae mchumba wake ambaye walipanga kuoana.
“Nimejaribu kuficha hii stori na kuufuta kichwani kwangu lakini imeshindikana, sikuopanda kuongea lakini nimeona ni wakati mwafka wa kusema, kile ambacho Rais jammeh alinifanyia ili Gambia na watu wengine wajue.
Yahya Jammeh aliikimbia nchi hiyo, Januari 2017 baada ya kushindwa katika Uchaguzi Mkuu na kukataa kutoka madarakani.
Mataifa ya Afrika Magharibi yaliingilia kati na Jammeh kutorokea Guinea Ya Ikweta ikiwa ni baada ya kukaa madarakani tangu mwaka 1994.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment