Search This Blog
Tuesday, November 12, 2019
Mbunge wa CCM ataka uzazi wa mpango kwa wanaume
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Khadija Nassir, ameitaka serikali kuanzisha programu za uzazi wa mpango kwa wanaume kwa kuwa utafiti mbalimbali unaonyesha wana uwezo wa kuwapa mimba wanawake tisa kwa siku moja.
Akiuliza swali la nyongeza bungeni, Mbunge huyo alisema utafiti mbalimbali duniani unaonesha kwamba mwanaume mmoja ana uwezo wa kuwapa mimba wanawake tisa kwa siku moja, wakati mwanamke mmoja ana uwezo wa kushika mimba moja kwa miezi tisa.
“Je, serikali haioni sasa kuendelea na program za uzazi wa mpango ni uharibifu wa rasilimali badala yake programu za uzazi wa mpango zifanyike kwa akina baba?”alihoji.
Akijibu, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk.Faustine Ndugulile, alisema ni dhana potofu kwamba uzazi wa mpango ni wanawake peke yao.
“Suala la uzazi wa mpango linawahusu wanaume vile vile na sisi kama serikali tunahamasisha kinababa na mama kushiriki kwenye uzazi wa mpango salama,” alisema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment