Search This Blog
Sunday, November 10, 2019
Marufuku kuuza ardhi iliyotolewa na Rais Magufuli - Waziri Lukuvi
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amekemea tabia ya Wananchi wa wilayani Kilosa kuuza mashamba yao waliyopewa na Rais John Pombe Magufuli mara baada ya kubatilishwa kutoka katika mashamba pori.
Waziri Lukuvi amekemea tabia hiyo alipokuwa wilayani Kilosa mkoani Morogoro katika ziara yake ya utatuzi wa migogoro ya ardhi.
Amesema baadhi ya wananchi wamekuwa wakiuza maeneo yao kwa tamaa ya pesa na mali halafu baadae wanaleta migogoro ya ardhi kwa kutaka mashamba mengine.
Wakati huo huo Wananchi wa kijiji cha Magomeni kilichopo tarafa ya Kilosa Mjini wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro wametoa kilio chao kwa Waziri Lukuvi wakitaka kupatiwa shamba la Mwekezaji Farm Africa Agro Focus Ltd marufu kama kwa Karamagi kwa madai kuwa mwekezaji wa shamba hilo ameshindwa kuliendeleza.
Wananchi hao wamemueleza Lukuvi kuwa kijiji hicho hakina ardhi ya kutosha kuwawezesha wananch hao kujishughulisha na kilimo na eneo kubwa katika kijiji hicho ni eneo la shamba la Farm lenye ukubwa wa ekari 13,000 ambapo Waziri Lukuvi alitatua hilo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment