Search This Blog
Sunday, November 24, 2019
JE, ni Maadili Baba Kumnunulia Bintiye ' Pedi ' na Kujua Kuwa Yupo Mwezini?
Siku hizi nimekuwa nikiwaona baadhi ya akina Baba ambao binafsi nawaita wa ' hovyo hovyo ' wakija na Mabinti zao tena wakubwa tu Madukani na hasa katika Supermarkets mbalimbali na kuwanunulia ' Pedi ' tena kuna wakati unakuta ' Li Dingi ' hilo hilo bila hata chembe ya aibu linamchangulia ' Bintiye ' aina ya ' taulo ' za kutumia.
Kama hii haitoshi hivi punde tu wakati na Mimi nikipanda Mti wangu nilioubatiza ' Le Mathematicien GENTAMYCINE ' niliweza kumsikia ' mubashara ' kabisa Baba mmoja akiongea na Simu na Mtu mwingine kuwa akimaliza tu kupanda Mti anataka kupitia dukani kumnunulia ' Bintiye ' taulo za Kike ' Pedi ' kwani alipotoka tu nyumbani kwake asubuhi hii alivyomuona tu alihisi kuwa ameanza safari yake ya kwenda ' Moon '.
Najua humu kuna akina Mama zetu na Wazee wenye MAADILI kabisa hivi haya mambo ya ' hovyo hovyo ' wayafanyayo Wazazi wa siku hizi hasa wa Kiume kwa Mabinti zao hususan kuwanunulia ' Pedi ' na kujua kuwa wapo ' Moon ' wamerithi kwenu nikimaanisha kuwa na nyie huko nyuma mlikuwa mkifanyiwa hivi au ni ' Uzungu ' tu umetuharibu na tunakosa maadili na kujua mipaka ya Baba juu ya Binti yake ambaye ni mkubwa na ameshavunja Ungo?
Badilikeni Wanaume wenzangu na akina Baba na jifunzeni kujua mipaka yenu hasa kwa Mabinti zenu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment