Search This Blog
Thursday, November 7, 2019
Diamond atoa somo kwa Wanafunzi
Kuelekea tamasha la Wasafi (Wasafi festival), msanii Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametembelea Shule ya Msingi Mwongozo kwaajili ya kutoa msaada na elimu ya virusi vya ukimwi.
Tukio hilo limetokea Alhamisi hii, ambapo baadhi ya shule za sekondari za jirani zimehudhuria ambazo Shule ya Sekondari ya Kambangwa Shule ya Sekondar Hananasifu, Shule ya Sekondari Turiani, Shule ya Sekondari Mzimuni na Shule ya Sekondari Makumbusho.
Akizungumza na wanafunzi hao Diamond amewataka kuongeza juhudi katika masomo yao na kujiepusha na mambo mabaya ikiwemo matumizi ya dawa za kulevya ili waweze kutimiza ndoto zao.
“Wasanii wengi wanatokea katika Wilaya ya Kinondoni hivyo jitahidini muyashikilie mazuri kuliko mabaya, mkitaka kufanikiwa zingatia kile unachokifanya, hapa kuna historia ya mambo ya mihadarati nisingependa kuwaona na nyie mkiingia huko,” amesema Diamond.
Kwa upande wake Mratibu wa Shughuli za kudhibiti ukimwi Halmashauri ya Kinondoni, Roby Gweso amewataka wanafunzi kuachana na tabia ya kutumia madawa ya kulevya na kuepuka vishawishi ili kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment