Search This Blog

Tuesday, October 22, 2019

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ashindwa kuunda baraza la mawaziri

Waziri mkuu wa Israel Bw. Benjamin Netanyahu ametangaza kushindwa kuunda baraza la mawaziri, na kurejesha mamlaka ya kufanya hivyo kwa rais Reuven Rivlin wa nchi hiyo. 

Amesema amefanya juhudi kujaribu kuunda serikali ya muungano yenye uwakilishi mkubwa, lakini ameshindwa kumshawishi kiongozi wa Chama cha Blue and White Bw. Benny Gantz kufanya mazungumzo naye. 

Taarifa iliyotolewa na ikulu ya nchi hiyo inasema rais Rivlin anapanga kumkabidhi Bw. Gantz jukumu la kuunda baraza la mawaziri, na atakuwa na muda wa siku 28 kufanya hivyo.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...