Search This Blog
Tuesday, October 8, 2019
Vikwazo 174 vya biashara EAC vimeondolewa kwa Wafanyabiashara
Jumla ya vikwazo 174 sawa na asilimia 75 vimeondolewa ili kurahisisha ufanyaji biashara kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo sasa itawezesha kuwepo kwa biashara kubwa baina ya nchi hizo.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam katika Ufunguzi wa Mkutano kati ya Wafanyabiashara na Kamati ya Taifa inayoshughulikia vikwazo vya biashara, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Mtangamano wa Biashara, Bi. Sekela Mwaisela alisema kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na kanda zingine kuna sheria ambazo zinazingitia biashara.
"Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Ibara ya 13(1) Itifaki ya Umoja wa Forodha ya Biashara pamoja na Ibara ya 6 ya Itifaki ya Biashara kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi zaKusini mwa Afrika (SADC) zinazitaka Nchi Wanachama kuondoa vikwazo vya zamani ili kuwezesha biashara kwa wafanyabiashara," Alisema Mwaisela.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment