Search This Blog
Monday, October 28, 2019
Naibu Spika aongoza Kamati ya Maazimio Chama cha Wabunge Wanawake wa Mabunge Jumuiya ya Madola
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson, ameongoza Kamati ya Maazimio ya Semina ya Wajumbe wa Chama cha Wabunge Wanawake wa Mabunge ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika uliofanyika Mkoani Arusha.
Katika Semina hiyo iliyofunguliwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan jana Oktoba 27, 2019 imepitisha maazimio mbalimbali yakiwemo:
Mosi; Mabunge Wanachama wa Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika yatunge na kuhakikisha zinatelekezwa sheria zitakazohakikisha vyama vya siasa vinazingatia usawa katika nafasi za uongozi; sheria zitakazozuia ama kuadhibu makosa yanayohusiana na ukatili na unyanyasaji wa wanawake kipindi chote cha uchaguzi.
Pili; Serikali za nchi husika zihakikishe kunakuwa na mtaala wa elimu kuhusu jinsia.
Tatu; Serikali husika na wadau wengine kuhakikisha inatolewa elimu juu ya masuala ya ushiriki wa wanawake katika uchaguzi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...



No comments:
Post a Comment