Search This Blog
Tuesday, October 29, 2019
Mwinyi Zahera Awatolea Uvivu Mashabiki wa Yanga
Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera amesema hawezi kuwasikiliza Mashabiki wanachokisema kwa sasa baada ya kufungwa na Pyramids FC kwani anawasiliana na Uongozi uliompa Mkataba
Ni baada ya mashabiki wa Klabu hiyo kulalamika wakimtaka Zahera kuondoka kutokana na matatizo wanayodai yamekithiri ikiwemo kushindwa kupanga kikosi na kukosa mbinu
"Mimi sikuajiriwa na mashabiki wa Yanga bali nilisaini mkataba na viongozi, kwa hiyo siku viongozi wakinitaka niwaachie timu nitafanya hivyo, sitokwenda mazoezini." ameeleza.
"Nina uzoefu mkubwa Afrika, mashabiki wanakasirika. Hakuna mchezaji yeyote wa Yanga anayeweza kucheza Pyramids na hatukusajili kwa ajili ya Klabu Bingwa ila ligi." Zahera alisisitiza.
Baada ya kufungwa na Pyramids FC goli 2-1 kutokea nchini Misri katika dimba la CCM Kirumba Mwanza, Yanga inahitaji ushindi wa magoli zaidi ya mawili ugenini ili kuweza kusonga mbele
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment