STAA grade one wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ humuambii kitu kwa mama wa mtoto wake mpya, Tanasha Donna Oketch kwa namna anavyomdekeza kama yai.
Tanasha kwa sasa anaishi maisha baabkubwa kwa kuwa baba wa mtoto wake huyo anamjali ile mbaya. Kwa mujibu wa vyanzo vya ndani ya familia ya Diamond au Mondi, Tanasha kuwa na jamaa huyo kama baba wa mtoto wake ni jambo la kifahari kwake hivyo anadeka kadiri atakavyo.
Baada ya kumzalia Mondi, sasa Tanasha ambaye ni mtangazaji na msanii wa muziki wa Kizazi Kipya anajiona kama malkia.
Kuthibitisha hilo, mapema wiki hii alitupia picha kwenye Insta Story akiringishia simu ya bei mbaya aliyonunuliwa na Mondi kama zawadi. Kufuatia zawadi hiyo, Tanasha alishindwa kujizuia na kujikuta akishukuru mno kwa zawadi hiyo;
“Nina furaha sana sasa hivi, asante Diamond Platinum kwa upendo wako kwangu.”
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment