Search This Blog

Monday, October 7, 2019

Mkurugenzi Mkuu Mstaafu wa Usalama wa Taifa afariki dunia


Mkurugenzi mkuu mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa (Tiss), Apson Mwang’onda (75) amefariki dunia jana nchini Afrika Kusini.

Taarifa za familia yake zinaeleza kuwa Mwang’onda alikuwa akisumbuliwa na saratani alilazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na baadaye kuhamishiwa Afrika Kusini.

Mwang’onda alikuwa mkurugenzi wa idara hiyo kuanzia mwaka 1995 hadi 2005, akiwa mkurugenzi wa sita wa idara hiyo tangu mwaka 1961.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...