Search This Blog
Wednesday, October 16, 2019
Mahakama Yaamuru Tanzania Kuilipa IPTL Sh426 bilioni
Dar es Salaam. kutokana na mgogoro uliopo kati ya Tanesco na kampuni ya IPTL, mahakama ya migogoro ya kimataifa (ICSID) imeiamuru Serikali ya Tanzania kulipa Dola 185.4 milioni (zaidi ya Sh426 bilioni) kwa kukiuka mkataba.
Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) liliingia makubaliano ya kuzalisha umeme na IPTL (Independent Power Tanzania Limited) mwaka 1995 lakini mwaka 2013 kukawa na kutoelewana kati ya wahusika wa mkataba huo.
NAFASI ZA AJIRA ZILIZOTANGAZWA LEO BONYEZA HAPA
Katika makubaliano hayo, IPTL iliyokuwa inamilikiwa kwa ubia kati ya kampuni ya Mechmar ya Malaysia na VIP Engineering and Marketing ya Tanzania ilitakiwa kuzalisha megawati 100 kwenye mitambo yake iliyosimikwa Tegeta jijini Dar es Salaam na kuiuzia Tanesco.
Kutekeleza mkataba huo, IPTL ilikopa fedha kutoka kwa taasisi tofauti za fedha zikiwamo benki za nchini Malaysia kwa ahadi ya kurejesha kutokana na mapato itakayokuwa inayapata ikilipwa na Tanesco.
Mwananchi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...

No comments:
Post a Comment