Search This Blog
Saturday, October 5, 2019
Magufuli Ajutia Kuwa Rais "Hii ni Kazi Ngumu SANA Hata Mawaziri Hawajui Kesho Yao"
RAIS John Magufuli amesema anajutia kwa kihelehela chake cha kujazafomu ya kugombea nafasi hiyo na amewaomba viongozi wa dini kumwombea kutoka na ugumu wa kazi alionayo
Magufuli amesema hayo leo Oktoba 4, 2019 wakati akiongea na wananchi wa mji Wa Mlowo mkoani Songwe kwenye ziara yake ya kikazi mkoani humo.
"Ndugu zangu kazi hii ni ngumu sana hata mawaziri wangu hawalali usingizi na hawajui kama kesho yake wataamka wakiwa katika nafasi zao," amesema.
Amesema kila unapoangalia kusonga mbele ujue kuna maadui sasa lazima tuchape kazi kwa kumtanguliza Mungu na wale waliojitoa ufahamu Mungu awasaidie.
"Eti mtu wa chama fulani anafurahia. ndege ya Tanzania kushikiliwa katika nchi nyingine, ninawaomba viongozi wa dini kubeba jukumu la kuliombea hilo," amesema Magufuli.
Pamoja na mambo mengine amesema serikali imetoa billion 18 kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe (SIA) na mkandarasi anaendelea na kazi, lengo likiwa ni kwa ndege kubwa kutua.
Vilevile rais Magufuli ameimiza upendo ,amani, ushirikiano kwa watanzania wote na kumtangyuliza Mungu kwa kila jambo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment