Search This Blog
Wednesday, October 30, 2019
Maaskofu Wapendekeza Wanaume Waliooa Kuwa Mapadre
MAASKOFU wa Kanisa Katoliki wapendekeza kuwaruhusu baadhi ya wanaume waliooa kufanya kazi za Upadre.
Pendekezo hili limepitishwa kwa kura 128 dhidi ya 41 zilizokataa. Hata hivyo lazima Papa Francis apitishe pendekezo hili na endapo liruhusiwa, basi hii itakuwa ni Historia kubwa ambayo itakuwa imewekwa na Kanisa hilo tangu kuanzishwa kwake.
Ruhusa hii itazihusu nchi za Bolivia, Brazil, Colombia, Ecuador, French Guiana, Guyana, Peru, Suriname, na Venezuela ambazo imethibitika kuwa kuna uhaba mkubwa wa Mpadre.
Kwa sasa kanisa hilo linaruhusu watu wasiooa tu ndiyo hupewa daraja takatifu la Upadre, lakini kwa Waanglikana wapo wanaoruhusiwa kuwa mapadre hata kama wameoa.
Katika mkutano Mkubwa wa Synod uliofanyika kwa wiki tatu na kumalizika Jumamosi iliyopita huko Vatican, ukihusisha maaskofu 184 kutoka sehemu mbalimbali duniani, masista na watumishi wengine wa kanisa hilo, walisema nchi za ukanda wa Amazon ndizo zinaathirika zaidi kwa kukosa mapadre kutokana na kikezo cha kutooa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment